Ruth Mnkeni na Aziza Juma, Dar es Salaam.
JUMLA ya Sh.bilioni 4.6 zinahitajika kwa ajili ya kuwasomesha wanafunzi wa walio
vyuoni ili kuboresha maendeleo katika sekta ya maji nchini.
Kauli hiyo ilitolewa Dar
es Salaam jana na Waziri wa Maji, Profesa Jumanne
Maghembe wakati wa kuzindua Mfuko wa Udhamini wa Maji (WTF) ambao unawasomesha wanafunzi wanaochukua
taaluma ya sekta ya maji.
Profesa Maghembe alisema kuwa mfuko huo utasaidia kuboresha
sekta hiyo kwani mahitaji ya maji ni makubwa katika maisha ya binadamu.
Aliongeza kusema kuwa wanao mpango mkakati wa kusambaza maji
katika maeneo ya vijijini kwani kuna vyanzo vingi ijapokuwa vinaathiriwa na
watu wachache kwa manufaa yao
binafsi .
“Kuna watu ambao ni wezi wa maji wanajitengenezea visima
wakidai kuwa vinatoa maji kumbe wanatumia maji ya DAWASCO lakini tulifanya
operesheni ya miezi mwili na tuliwakamata zaidi ya watu 90 ambao walikuwa
wanaiba maji,”alisema
“Juhudi hizi zimepelekea sehemu nyingi katika jiji la Dar es
Salaam kupata maji tofauti na ilivyokuwa awali kwani baadhi yao wamehukumiwa na wengine kesi zinaendelea
katika mahakama ya jiji .
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Mfuko huo Dayana Mwiru alisema
lengo la kuanzisha mfuko huo ni kujaribu kuongeza idadi ya wanataaluma wa sekta
ya maji kwani ni wachache mno.
Alisema utafiti uliofanywa mwaka 2011 ulionyesha kuwa
mahitaji ya maji yanahitaji wanataaluma 3000 ili kuweza kufanya kazi ipasavyo
tofauti na sasa ambapo haikidhi kwani kuna chuo kimoja tu kinachotoa taaluma
hiyo na kwa sasa kuna wanafunzi 1600 ambao wapo kwenye taaluma hiyo.
“Mfuko huu utasaidia kwenya idadi ya wanafunzi kwa kuangalia
usawa wa jinsia, watu wanaotoka katika familia duni na pia wanawake kuwapa kipaumbele ili kuhakikisha
kuwa wanafikia malengo bila kujali anatoka katika falimilia gani,”alisema
Mwiru.
No comments:
Post a Comment