Aziza Juma
na Anolina Herman, Dar es Salaam.
JESHI la
polisi kanda maalum ya Dar es Salaam limefanya msako na kufanikiwa kuwakamata
watu watano wakiwa na milipuko hatari katika msako unaoendelea jijini Dar es
Salaam.
Akizumza
Kamanda wa polisi kanda maalum Dar es Salaam Suleymani Kova alisema kuwa msako huo
ulifanyika maeneo ya kunduchi na kukamata kundi moja linalojishughulisha na maswala ya
milipuko na kumiliki vifaa vya milipuko bila ya kibali kitoka Polisi.
Alisema Kova
watuhumiwa hao wametajwa kuwa ni Juma Khaluifani (24), Ruben Patrick(26),Happy
Charles(28), Sadick Seif(32)na Iddi Shabani(40) wote ni wakazi wa Mtongani
Jijini Dar es Salaam.
Alisema Kova
watuhumiwa hao walikutwa na vifaa mbalimbali vya milipuko nyaya 62 za milipuko zikiwa
zimefungwa betri,nyaya ndefu mizunguko minne ,tyubu 20 za urefu wa sentimita 30
zilizojazwa mbolea ya urea na tambi rola 1 .
“Vifaa vyote
hivyo ni hatari na vikiunganishwa vinaweza kuhatarisha maisha ya watu na mali
zao”,alisema Kova
Pia alisema
watumiwa haohao walikutwa na dawa za kulevya aina ya bhangi gunia moja.
Alimalizia
kwakusema kuwa uchunguzi zaidi unafanyika ili kujua madhumumi halisi ya
watuhumiwa hao katika kumiliki vifaa saidizi na milipuko hiyo hatari.
No comments:
Post a Comment