Saturday, May 18, 2013

Jeshi la Polisi laokoa shaba ikiwa inatoroshwa.


Adelina Rutale na Aziza Juma, Dar es Salaam
JESHI la polisi Kanda Maalum limefanikiwa kukamata vipande 650 vya Shaba vilivyokuwa vikisafirishwa kutoka nchini Zambia kuja bandari ya Dar es Salaam.

Akizungumza jijijini Dar es Salaam jana Kamanda wa polisi Kanda Maalumu Suleiman Kova alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari alisema kuwa katika msako huo pia walifanikiwa kukamata meno ya tembo 27,  ngozi nne za chui na fedha bandia zenye thamani ya shilingi milioni saba.

Alisema kuwa wamefanikiwa kuwakamata watuhumiwa saba ambao watafikishwa mahakamani muda wowote ili kujibu mashitaka yanayowakabili.

“Jeshi la polisi limefanya kazi ya msako ambapo tumeweza kuwakamata watuhumiwa hao saba wakiwa na mali mbalimbali kinyume na sheria,

“Tunaendelea na uchunguzi wa kina ili kuendelea kukamata wahalifu wanaosafirisha mali za watanzania,”alisema Kova.

Pia Kova alisema kuwa katika msako huo walifanikiwa kukamata feni 50,bunduki moja aina ya SMG ikiwa na namba  2608997 ikiwa na magazine na gari aina ya SUZUKI CARRY yenye  namba za usajili  T 289 BYL huko maeneo ya Kibangulile mkoa wa Temeke.

No comments:

Post a Comment