Friday, May 24, 2013

Lipsticki, lipshine zenye madini ya sumu



Wanawake hupenda kuonekana nadhifu sikuzote na katika kufanya hivyo wanatumia vitu mbalimbali vikiwamo rangi za aina mbalimbali ambazo baadhi yake hupakwa katika miili yao ikiwamo midomo.
Rangi na mafuta ya midomo ambayo hutumiwa zaidi na wanawake yanaelezwa kuwa na sumu ambayo huweza kusababisha saratani ya mapafu, kushindwa kwa figo kufanya kazi na hata maumivu ya tumbo.
Utafiti uliochapishwa  Januari mwaka huu na Jarida la Sayansi ya Mazingira nchini Uingereza (JES) umebaini kuwa  matumizi ya muda mrefu ya rangi za midomo na ‘lipglosses’ yanaweza kusababisha maradhi kadhaa kutokana na kuwa na kiwango cha madini ya aluminiam, cadmium na risasi (lead).
Kemikali zinazopatikana zaidi katika rangi za midomo zinatajwa kuwa ni cadmium, chromium, titanium, lead na manganizi.
Ingawa bidhaa hasa zenye wingi wa madini hayo hazijawekwa wazi,wanasayansi hao wanasema kuwa ni zile zinazotumiwa au kupendwa zaidi na kinamama.
Imebainika kuwa kupaka ‘lipshine’ au ‘lipstick’ mara tatu na zaidi kwa siku kunaweza kusababisha maradhi hayo na ilishauriwa kuwa matumizi yake yasiwe ya muda mrefu.
Mkuu wa utafiti huu, Katharine Hammond, mwanasayansi wa mazingira na afya katika Chuo Kikuu cha California, Marekani   anasema nia ya utafiti huo ni kutaka kupima kiwango cha madini hayo ambacho mtumiaji wa lipstiki huweza kukimeza na kiwango kinachokubalika.
“Kiafya,  mtumiaji hatakiwi kunywa au kumeza zaidi ya asilimia 20 ya metali za lead au cadmonium hata katika maji tu ya kunywa,” anasema Hammond
 Utafiti wa Hammond unaeleza kuwa bidhaa hizo zina kiwango kikubwa cha aluminium, cadmium, chromium na manganizi kilichozidi asilimia 20.
 Hali ikoje nchini
 Afisa Uhusiano wa Mamlaka ya Chakula na Madawa(TFDA) Gaudensia Simwanza anasema  madini ya Lead na Titanium yapo kwenye orodha ya mchanganyiko uliozuiwa.
“Lakini madini ya titanium dioxide ndiyo yanaruhusiwa na siyo titanium zote” anasema Simwanza
 source: Lipstiki--lipshine-zenye-madini-ya-sumu

No comments:

Post a Comment