Saturday, May 18, 2013

Waziri Charlote Slen wa Denmark aishauri TRA kuhusu misamaha ya kodi.


Na Christina Gauluhanga, Dar es Salaam

NAIBU Waziri wa Ushirikiano na Maendeleo wa Serikali ya Denmark, Charlote Slen ameishauri Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), ihakikishe misamaha ya kodi inalenga  kuwapunguzia wananchi umaskini na kuleta usawa.

Kauli hiyo imetolewa Dar es Salaam jana na Naibu Waziri Slen alipotembelea TRA nchini hapa ambapo amekuja nchini hapa kwa ziara ya kiserikali na alifika TRA ili kufahamu mamlaka hiyo ina mpango gani wa miaka mitano ijayokwa lengo la kupunguza umaskini Tanzania.

Alisema mfano kwa Serikali ya Denmark inahakikisha misamaha ya kodi ni sawa kwa sawa hivyo imesaidia kupunguza umaskini kwa kutumia mbinu mbalimbali za kisasa.

Hata hivyo Kamishna Mkuu wa TRA, Harry Kitillya alisema dhamira hiyo itatekelezwa kwakuwa serikali iliweka lengo hilo hivyo ana imani litatekelezeka.

Kitillya alisema tangu kuanza kutumika kwa mashine hizo katika awamu ya kwanza wafanyabiashara 14,800 wamejiunga na mfumo huo sawa na asilimia 92.

Alisema kutokana na mwamko huo wamehakikisha wanapata wasambazaji wa kutosha wa mashine hizo na karatasi pamoja na kutoa mafunzo mbalimbali kwa watendaji ili kuondoa changamoyo zikazojitokeza.

Alisema serikali ilianzisha mfumo huo Julai mwaka 2010 lwa nego la kuboresha kumbukumbu za wafanyabiashara wanaotoza na kukusanya kodi za Ongezeko la Thamani (VAT), ambapo awamu ya pili iliyozinduliwa jana inawahusu wafanyabiashara ambao hawatozi VAT.

“ Awamu hii imelenga kuanza na kundi la wafanyabiashara wapatao 200,000 wenye mauzo ghafi yenye thamani ya Sh Mil 14 kwa mwaka,”alisema Kitillya.

Kitillya alisema tangu kuanza kutumika kwa mashine hizo kwa miaka miwili sasa wameona mafanikio ambapo takwimu zinaonesha kuwa kwa mwaka wa kwanza wa utekelezaji mfumo huo wamekusanya makusanyo yatokanayo an VAT yalikuwa asilimia 9 na kufikia asilimia 23.

Naye Naibu Kamishna wa Kodi, Rished Bade  alisema mashine hizo zimetengenezwa kwa kuzingatia faida anazoweza kuzipata mtumiaji katika uendeshaji wa biashara yake.

Alisema ili kurahisisha upatikanaji wa mashine hizo, TRA imeingia makubaliano na kusaini mikataba na makampuni 11 ambayo yatasambaza na kutoa elimu kwa watumiaji wa mashine hizo.

Pia kampuni nne zimeteuliwa kusambaza karatasi zenye ubora wa kutoa risiti zisizofutika ambazo zinatumiwa na mashine hizo.

No comments:

Post a Comment