Saturday, May 18, 2013

75% ya watanzania wajihusisha na shughuli zilizo katika sekta isiyo rasmi.

 Adelina Rutale na Aziza Juma, Dar es Salaam
 IMEELEZWA kuwa zaidi ya asilimia 75 ya watanzania wenye uwezo wa kufanya kazi wanajihusisha na shughuli zilizopo katika sekta isiyo rasmi ili kujipatia kipato chao.

Kauli hiyo imetolewa baada ya kiwango kikubwa cha ukosefu wa ajira nchini kinazidi kushika kasi hali ambayo imeendelea kuzitesa nchi zinazoendelea za afrika mashariki na kusini mwa jangwa la Sahara.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana  Mkurugenzi wa Idara ya Kazi na Ajira katika Wizara ya  Kazi na Ajira Ally Msangi kwa niaba ya Katibu Mkuu wa wizara hiyo Erick Shitindi katika kikao kilichowakutanisha wadau mbalimbali  kujadili hali ya soko la ajira duniani.

Msangi alisema kuwa utafiti huo utagusa sehemu kubwa ya nguvu kazi na utaiwezesha serikali kupata picha halisi ya hali ya ajira nchini,utafiti huo hutoa taarifa kuhusu hali ya ajira nchini katika sekta isiyo rasmi,utumikishwaji wa watoto,hali ya hifadhi ya jamii,hali ya kipato nchini na matumizi ya muda na ajira mpya zilizozalishwa katika sekta zote kwa kipindi husika (2006-2013).

“Katika kufikia dira ya maendeleo ya taifa (vision 2025) Tanzania imejiwekea mikakati mbalimbali ikiwemo mkakati wa kukuza uchumi na kupunguza umaskini Tanzania(MKUKUTA) wenye malengo ya kuhakikisha kiwango cha ukosefu wa ajira kinapungua,utumikishwaji wa watoto unapungua na ajira isiyotimilifu inapungua.

“Utafiti huu pekee wa hali ya nguvu kazi nchini ndio unaweza kutoa hali halisi ya viashiria hivyo ili kufikia malengo na maendeleo tunayoyahitaji,”alisema Msangi.

Alisema kuwa kwa sasa imebaki miaka miwili kufikia hitimisho la tathmini ya malengo ya maendeleo ya millenia (MDGs) mwaka 2015 ambapo nchi inapaswa kutoa taarifa ya viwango vya viashiria vya malengo hayo hususani katika MDGs.
“Wote ni wadau nuhimu katika mchakato huu kwa kuwa masuala ya ajira na kazi ni masuala mtambuka ambayo juhudi za pamoja zinahitajika kati ya serikali,taasisi za elimu,taasisi za utafiti,wawekezaji,mashirika yasiyo ya serikali,wabia wa maendeleo,waandishi wa habari na wananchi kwa ujumla ili kufikia malengo tuliyojiwekea,”alisema Msangi.

No comments:

Post a Comment