Friday, May 24, 2013

Pic of the day. Foods that help fight Diabetes

FOODS THAT HELP FIGHT DIABETES

In order to control Type I or Type II diabetes, it is imperative that those with this metabolic disease follow a stringent nutritional plan. In general, the foods that help diabetes have a low glycemic index (a ranked score less than fifty-five for carbohydrates that slightly elevate blood glucose) and provide key nutrients such as calcium, potassium, fiber, magnesium, and vitamin A, C and E. More specifically there are certain foods that help diabetics cope with their condition.

BEANS


Beans are starchy foods that not only satisfy energy and protein needs while burning fat, but they also help

moderate blood levels of glucose and insulin. Beans contain the highest percentages of resistant starches, dietary carbohydrates that resist digestion and pass through to the large intestine, according to Chetday.com. According

to Karen Collins, M.S., R.D., C.D.N., a nutrition adviser to the American Institute for Cancer Research, in Washington, D.C., the soluble fiber within beans binds to carbohydrates and slows their digestion which then

prevents spikes in blood glucose. In addition, the antioxidant pigments found in beans inhibit inflammation from dietary sugars and starches.


DARK GREEN LEAFY VEGETABLES


According to a study conducted at Tulane University, eating lots of green leafy vegetables such as spinach, collards and kale daily may help reduce the risk of developing diabetes. Results from the study showed a nine percent reduction in diabetes risk with every additional serving of green leafy vegetables

SWEET POTATOES


Sweet potatoes are a starchy vegetable containing a healthy dose of vitamin A and fiber. Replace regular potatoes with sweet potatoes for a lower glycemic index alternative.




 
BERRIES

A variety of berries including blueberries, strawberries and raspberries provide antioxidants, vitamins C, fiber, folic acid and powerful antioxidants. Berries are low in calories and fat and do not spike blood sugar because of their low carbohydrate content.

TOMATOES


Eating tomatoes help to reduce escalating inflammation brought on by diabetes. In addition, tomatoes are a great source of antioxidants (especially lycopene which is found in tomatoes), fiber, iron, and vitamins A, C and E. These nutrients play a large role in regulating blood sugar levels in the body.

FISH HIGH IN OMEGA-3 FATTY ACIDS


Eat six to nine ounces of fish per week. Salmon is highly recommended as a good source of omega-3 fatty acids. Diabetes is the leading cause of end-stage kidney disease. A study conducted in England involving 22,300 adults determined that eating at least two servings of fish each week seems to protect people with diabetes who also have kidney disease. The study, cited in "USA Today", showed that fish consumption lowers abnormal levels of protein in the urine in people with diabetes.

WHOLE GRAINS


Eating whole grains such as oatmeal, barley and bran supplies the body with high quality sources of magnesium, chromium, omega-3 fatty acids, foliate, fiber and potassium. These nutrients are responsible for regulating blood sugar within the body and giving whole grain foods a low glycemic index.

NUTS


Nuts such as walnuts, flax seeds and almonds contain magnesium, fiber and omega-3 fatty acids. Eat an ounce of nuts as a snack once a day to help keep blood sugar leveled and keep hunger controlled

Lipsticki, lipshine zenye madini ya sumu



Wanawake hupenda kuonekana nadhifu sikuzote na katika kufanya hivyo wanatumia vitu mbalimbali vikiwamo rangi za aina mbalimbali ambazo baadhi yake hupakwa katika miili yao ikiwamo midomo.
Rangi na mafuta ya midomo ambayo hutumiwa zaidi na wanawake yanaelezwa kuwa na sumu ambayo huweza kusababisha saratani ya mapafu, kushindwa kwa figo kufanya kazi na hata maumivu ya tumbo.
Utafiti uliochapishwa  Januari mwaka huu na Jarida la Sayansi ya Mazingira nchini Uingereza (JES) umebaini kuwa  matumizi ya muda mrefu ya rangi za midomo na ‘lipglosses’ yanaweza kusababisha maradhi kadhaa kutokana na kuwa na kiwango cha madini ya aluminiam, cadmium na risasi (lead).
Kemikali zinazopatikana zaidi katika rangi za midomo zinatajwa kuwa ni cadmium, chromium, titanium, lead na manganizi.
Ingawa bidhaa hasa zenye wingi wa madini hayo hazijawekwa wazi,wanasayansi hao wanasema kuwa ni zile zinazotumiwa au kupendwa zaidi na kinamama.
Imebainika kuwa kupaka ‘lipshine’ au ‘lipstick’ mara tatu na zaidi kwa siku kunaweza kusababisha maradhi hayo na ilishauriwa kuwa matumizi yake yasiwe ya muda mrefu.
Mkuu wa utafiti huu, Katharine Hammond, mwanasayansi wa mazingira na afya katika Chuo Kikuu cha California, Marekani   anasema nia ya utafiti huo ni kutaka kupima kiwango cha madini hayo ambacho mtumiaji wa lipstiki huweza kukimeza na kiwango kinachokubalika.
“Kiafya,  mtumiaji hatakiwi kunywa au kumeza zaidi ya asilimia 20 ya metali za lead au cadmonium hata katika maji tu ya kunywa,” anasema Hammond
 Utafiti wa Hammond unaeleza kuwa bidhaa hizo zina kiwango kikubwa cha aluminium, cadmium, chromium na manganizi kilichozidi asilimia 20.
 Hali ikoje nchini
 Afisa Uhusiano wa Mamlaka ya Chakula na Madawa(TFDA) Gaudensia Simwanza anasema  madini ya Lead na Titanium yapo kwenye orodha ya mchanganyiko uliozuiwa.
“Lakini madini ya titanium dioxide ndiyo yanaruhusiwa na siyo titanium zote” anasema Simwanza
 source: Lipstiki--lipshine-zenye-madini-ya-sumu

Faida za tikitiki maji kiafya.


Baadhi ya vyakula vimekuwa vikifurahisha pale vinapoliwa, tikiti maji ni miongoni mwa vyakula hivyo. Kwanza ule mchanganyiko wa rangi zake hulifanya sio tu kuvutia bali kuwa kama ua lililochanua juu ya meza ya mlaji husika.
Kama vile haitoshi tunda hili limejaaliwa virutubisho kadha wa kadha vyenye faida kubwa katika afya ya mwanadamu.
Licha ya 92% ya tikiti maji kuwa ni maji, bado zile 8% zilizobaki zina faida kubwa sana kiafya jambo linaloonekana kutofahamika kwa wengi. Zifuatazo ni baadhi tu ya faida chache kati ya nyingi za tunda hili la tikiti maji:
Tikiti maji ni chanzo kizuri cha vitamini. Katika tunda hilo kuna Vitamin A, inayosaidia kuboresha afya ya macho na pia kuondosha sumu mwilini; Vitamin C, inayosaidia kuboresha kinga, kuponya majeraha, kukinga uharifu wa seli, kuboresha afya meno na fizi;  na vitamini B6, inayosaidia ubongo kufanya kazi na pia kuibadilisha protini kuwa nishati.
  Tunda la tikiti maji lina kiwango kikubwa cha  lycopene kuliko tunda lolote au mboga za majani.
Ikiwa familia yako inaishi kwenye eneo lisilo na vyanzo vya madini ya potasium, unaweza kuwapa tikiti badala yake. Lina uwezo mkubwa wa kusaidia misuli na mfumo wa fahamu kwa ujumla kufanya kazi zake vizuri.
 Halikadhalika tunda hili huweza kukuondoa katika hatari ya kupata shinikizo la damu.
Tikiti pia lina  amino asidi na virutubisho vingine vinavyosaidia kurahisisha mtiririko wa damu kwenye mishipa yake.
Sifa ya kipekee iliyopo katika tunda hili, ni ule uwezo wake wa kusaidia kupunguza ama kuondoa tatizo la upungufu wa nguvu za kiume. Kwa kunywa juisi yake iliyokamuliwa bila kumenywa kwa maganda yake, kutaisadia kabisa kuondoa tatizo hilo.
Kwa kawaida tunda hili huliwa  peke yake au kwa kuchanganya na matunda mengine. Kwa mujibu wa wataalamu wa mambo ya afya ya vyakula kila kitu kwenye tikiti maji kina faida kiafya ukianzia kwenye majani tunda na hata nyama yake.
source: Faida za tikitiki maji. 

Saturday, May 18, 2013

Milipuko hatari yakamatwa Dar es salaam.



Aziza Juma na Anolina Herman, Dar es Salaam.

JESHI la polisi kanda maalum ya Dar es Salaam limefanya msako na kufanikiwa kuwakamata watu watano wakiwa na milipuko hatari katika msako unaoendelea jijini Dar es Salaam.  

Akizumza Kamanda wa polisi kanda maalum Dar es Salaam  Suleymani Kova alisema kuwa msako huo ulifanyika maeneo ya kunduchi na kukamata  kundi moja linalojishughulisha na maswala ya milipuko na kumiliki vifaa vya milipuko bila ya kibali kitoka Polisi. 

Alisema Kova watuhumiwa hao wametajwa kuwa ni Juma Khaluifani (24), Ruben Patrick(26),Happy Charles(28), Sadick Seif(32)na Iddi Shabani(40) wote ni wakazi wa Mtongani Jijini Dar es Salaam.

Alisema Kova watuhumiwa hao walikutwa na vifaa mbalimbali vya milipuko nyaya 62 za milipuko zikiwa zimefungwa betri,nyaya ndefu mizunguko minne ,tyubu 20 za urefu wa sentimita 30 zilizojazwa mbolea ya urea na tambi rola 1 .

“Vifaa vyote hivyo ni hatari na vikiunganishwa vinaweza kuhatarisha maisha ya watu na mali zao”,alisema Kova

Pia alisema watumiwa haohao walikutwa na dawa za kulevya aina ya bhangi gunia moja.
Alimalizia kwakusema kuwa uchunguzi zaidi unafanyika ili kujua madhumumi halisi ya watuhumiwa hao katika kumiliki vifaa saidizi na milipuko hiyo hatari.

Wizara ya Maji inahitaji Sh.bilion 4.6 kusomesha wataalamu wa maji.


Ruth Mnkeni na Aziza Juma, Dar es Salaam.

JUMLA ya Sh.bilioni 4.6 zinahitajika  kwa ajili ya kuwasomesha wanafunzi wa walio vyuoni ili kuboresha maendeleo katika sekta ya maji nchini.

Kauli hiyo ilitolewa Dar es Salaam jana na Waziri wa Maji, Profesa Jumanne Maghembe wakati wa kuzindua Mfuko wa Udhamini wa Maji (WTF)  ambao unawasomesha wanafunzi wanaochukua taaluma ya sekta ya maji.

Profesa Maghembe alisema kuwa mfuko huo utasaidia kuboresha sekta hiyo kwani mahitaji ya maji ni makubwa katika maisha ya binadamu.

Aliongeza kusema kuwa wanao mpango mkakati wa kusambaza maji katika maeneo ya vijijini kwani kuna vyanzo vingi ijapokuwa vinaathiriwa na watu wachache kwa manufaa yao binafsi .

“Kuna watu ambao ni wezi wa maji wanajitengenezea visima wakidai kuwa vinatoa maji kumbe wanatumia maji ya DAWASCO lakini tulifanya operesheni ya miezi mwili na tuliwakamata zaidi ya watu 90 ambao walikuwa wanaiba maji,”alisema

“Juhudi hizi zimepelekea sehemu nyingi katika jiji la Dar es Salaam kupata maji tofauti na ilivyokuwa awali kwani baadhi yao wamehukumiwa na wengine kesi zinaendelea katika mahakama ya jiji .

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Mfuko huo Dayana Mwiru alisema lengo la kuanzisha mfuko huo ni kujaribu kuongeza idadi ya wanataaluma wa sekta ya maji kwani ni wachache mno.

Alisema utafiti uliofanywa mwaka 2011 ulionyesha kuwa mahitaji ya maji yanahitaji wanataaluma 3000 ili kuweza kufanya kazi ipasavyo tofauti na sasa ambapo haikidhi kwani kuna chuo kimoja tu kinachotoa taaluma hiyo na kwa sasa kuna wanafunzi 1600 ambao wapo kwenye taaluma hiyo.

“Mfuko huu utasaidia kwenya idadi ya wanafunzi kwa kuangalia usawa wa jinsia, watu wanaotoka katika familia duni na pia  wanawake kuwapa kipaumbele ili kuhakikisha kuwa wanafikia malengo bila kujali anatoka katika falimilia gani,”alisema Mwiru.

75% ya watanzania wajihusisha na shughuli zilizo katika sekta isiyo rasmi.

 Adelina Rutale na Aziza Juma, Dar es Salaam
 IMEELEZWA kuwa zaidi ya asilimia 75 ya watanzania wenye uwezo wa kufanya kazi wanajihusisha na shughuli zilizopo katika sekta isiyo rasmi ili kujipatia kipato chao.

Kauli hiyo imetolewa baada ya kiwango kikubwa cha ukosefu wa ajira nchini kinazidi kushika kasi hali ambayo imeendelea kuzitesa nchi zinazoendelea za afrika mashariki na kusini mwa jangwa la Sahara.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana  Mkurugenzi wa Idara ya Kazi na Ajira katika Wizara ya  Kazi na Ajira Ally Msangi kwa niaba ya Katibu Mkuu wa wizara hiyo Erick Shitindi katika kikao kilichowakutanisha wadau mbalimbali  kujadili hali ya soko la ajira duniani.

Msangi alisema kuwa utafiti huo utagusa sehemu kubwa ya nguvu kazi na utaiwezesha serikali kupata picha halisi ya hali ya ajira nchini,utafiti huo hutoa taarifa kuhusu hali ya ajira nchini katika sekta isiyo rasmi,utumikishwaji wa watoto,hali ya hifadhi ya jamii,hali ya kipato nchini na matumizi ya muda na ajira mpya zilizozalishwa katika sekta zote kwa kipindi husika (2006-2013).

“Katika kufikia dira ya maendeleo ya taifa (vision 2025) Tanzania imejiwekea mikakati mbalimbali ikiwemo mkakati wa kukuza uchumi na kupunguza umaskini Tanzania(MKUKUTA) wenye malengo ya kuhakikisha kiwango cha ukosefu wa ajira kinapungua,utumikishwaji wa watoto unapungua na ajira isiyotimilifu inapungua.

“Utafiti huu pekee wa hali ya nguvu kazi nchini ndio unaweza kutoa hali halisi ya viashiria hivyo ili kufikia malengo na maendeleo tunayoyahitaji,”alisema Msangi.

Alisema kuwa kwa sasa imebaki miaka miwili kufikia hitimisho la tathmini ya malengo ya maendeleo ya millenia (MDGs) mwaka 2015 ambapo nchi inapaswa kutoa taarifa ya viwango vya viashiria vya malengo hayo hususani katika MDGs.
“Wote ni wadau nuhimu katika mchakato huu kwa kuwa masuala ya ajira na kazi ni masuala mtambuka ambayo juhudi za pamoja zinahitajika kati ya serikali,taasisi za elimu,taasisi za utafiti,wawekezaji,mashirika yasiyo ya serikali,wabia wa maendeleo,waandishi wa habari na wananchi kwa ujumla ili kufikia malengo tuliyojiwekea,”alisema Msangi.

Waziri Charlote Slen wa Denmark aishauri TRA kuhusu misamaha ya kodi.


Na Christina Gauluhanga, Dar es Salaam

NAIBU Waziri wa Ushirikiano na Maendeleo wa Serikali ya Denmark, Charlote Slen ameishauri Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), ihakikishe misamaha ya kodi inalenga  kuwapunguzia wananchi umaskini na kuleta usawa.

Kauli hiyo imetolewa Dar es Salaam jana na Naibu Waziri Slen alipotembelea TRA nchini hapa ambapo amekuja nchini hapa kwa ziara ya kiserikali na alifika TRA ili kufahamu mamlaka hiyo ina mpango gani wa miaka mitano ijayokwa lengo la kupunguza umaskini Tanzania.

Alisema mfano kwa Serikali ya Denmark inahakikisha misamaha ya kodi ni sawa kwa sawa hivyo imesaidia kupunguza umaskini kwa kutumia mbinu mbalimbali za kisasa.

Hata hivyo Kamishna Mkuu wa TRA, Harry Kitillya alisema dhamira hiyo itatekelezwa kwakuwa serikali iliweka lengo hilo hivyo ana imani litatekelezeka.

Kitillya alisema tangu kuanza kutumika kwa mashine hizo katika awamu ya kwanza wafanyabiashara 14,800 wamejiunga na mfumo huo sawa na asilimia 92.

Alisema kutokana na mwamko huo wamehakikisha wanapata wasambazaji wa kutosha wa mashine hizo na karatasi pamoja na kutoa mafunzo mbalimbali kwa watendaji ili kuondoa changamoyo zikazojitokeza.

Alisema serikali ilianzisha mfumo huo Julai mwaka 2010 lwa nego la kuboresha kumbukumbu za wafanyabiashara wanaotoza na kukusanya kodi za Ongezeko la Thamani (VAT), ambapo awamu ya pili iliyozinduliwa jana inawahusu wafanyabiashara ambao hawatozi VAT.

“ Awamu hii imelenga kuanza na kundi la wafanyabiashara wapatao 200,000 wenye mauzo ghafi yenye thamani ya Sh Mil 14 kwa mwaka,”alisema Kitillya.

Kitillya alisema tangu kuanza kutumika kwa mashine hizo kwa miaka miwili sasa wameona mafanikio ambapo takwimu zinaonesha kuwa kwa mwaka wa kwanza wa utekelezaji mfumo huo wamekusanya makusanyo yatokanayo an VAT yalikuwa asilimia 9 na kufikia asilimia 23.

Naye Naibu Kamishna wa Kodi, Rished Bade  alisema mashine hizo zimetengenezwa kwa kuzingatia faida anazoweza kuzipata mtumiaji katika uendeshaji wa biashara yake.

Alisema ili kurahisisha upatikanaji wa mashine hizo, TRA imeingia makubaliano na kusaini mikataba na makampuni 11 ambayo yatasambaza na kutoa elimu kwa watumiaji wa mashine hizo.

Pia kampuni nne zimeteuliwa kusambaza karatasi zenye ubora wa kutoa risiti zisizofutika ambazo zinatumiwa na mashine hizo.

Jeshi la Polisi laokoa shaba ikiwa inatoroshwa.


Adelina Rutale na Aziza Juma, Dar es Salaam
JESHI la polisi Kanda Maalum limefanikiwa kukamata vipande 650 vya Shaba vilivyokuwa vikisafirishwa kutoka nchini Zambia kuja bandari ya Dar es Salaam.

Akizungumza jijijini Dar es Salaam jana Kamanda wa polisi Kanda Maalumu Suleiman Kova alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari alisema kuwa katika msako huo pia walifanikiwa kukamata meno ya tembo 27,  ngozi nne za chui na fedha bandia zenye thamani ya shilingi milioni saba.

Alisema kuwa wamefanikiwa kuwakamata watuhumiwa saba ambao watafikishwa mahakamani muda wowote ili kujibu mashitaka yanayowakabili.

“Jeshi la polisi limefanya kazi ya msako ambapo tumeweza kuwakamata watuhumiwa hao saba wakiwa na mali mbalimbali kinyume na sheria,

“Tunaendelea na uchunguzi wa kina ili kuendelea kukamata wahalifu wanaosafirisha mali za watanzania,”alisema Kova.

Pia Kova alisema kuwa katika msako huo walifanikiwa kukamata feni 50,bunduki moja aina ya SMG ikiwa na namba  2608997 ikiwa na magazine na gari aina ya SUZUKI CARRY yenye  namba za usajili  T 289 BYL huko maeneo ya Kibangulile mkoa wa Temeke.