Thursday, June 6, 2013

Wafanyabiashara wa vifaa vya ujenzi waishauri TRA kupunguza bei ya mashine za kutolea risiti.



Na Aziza Juma, Dar ea Salaam.

WAFANYABIASHARA wa vifaa vya ujenzi wameishauri Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kupunguza bei ya mashine za kutolea risiti ili wafanyabiashara wote kumudu kununua mashine hizo.

Akizungimza na MTANZANIA jana  mmoja wa wafanyabiashara hao Matchowea Malisa katika semina ya wafanyabiashara inayoendelea katika wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam.

Malisa alisema kuwa wafanyabiashara wengi wanatumia mikopo kuendesha biashara zao hivyo itakuwa vigumu kutafuta rejesho la mkopo benk wakati huhuo anatakiwa kununua mashine ambayo inauzwa bei  kubwa kiasi cha laki nane.

Alisema pamoja mashine zina faida kubwa na nyingi sana lakini zinafanya kazi taratibu sana hali inayopelekea ugumu wateja wanapokiwa zaidi ya wawili.

Pia Malisa alisema kuwa watengenezaji wa bedhaa na wafanyabiashara wa jumla waseuza rejareja bidhaa wanazotengeneza ili kuwapa nafasi ya wale wanaouza rejareja tu waweze kuuza kwani wateja wote wanakimbilia huko kwakua bei yao ya chini sana.

Aliongezea kuwa msamaha wa kodi kwa wafanyabiashara wenyemtaji mdogo usiozidi milioni nne unapunguza uzalendo kwani watakuwa hawana uchungu na nchi yao pia hawato changia
ongezeko la pato la Taifa.

No comments:

Post a Comment