Thursday, June 6, 2013

Mkuu Wa Mkoa Dar ataka wananchi waishio mabondeni wasipimiwe viwanja vyao.



Adelina Rutale na Maneno Selanyika,Dar es Salaam

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadick amewataka viongozi wa mipango miji kutokuwapimia viwanja wananchi maeneo ya mabondeni ambayo ni hatari kwa maisha yao baada ya mafuriko kutokea.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana wakati wa kuhitimisha siku ya maadhimisho ya Mazingira Duniani Sadick alisema kuwa baadhi ya viongozi wamekuwa wakijichukulia sheria ya kupima viwanja maeneo ya mabondeni kinyume na sheria.

Pia alisema kuwa wananchi wamekuwa mstari wa mbele kuharibu mazingira kwa kuchimba michanga na kokoto maeneo mbalimbali ya hapa Dar es salaam na kusababisha adha ya mazingira kuwa machafu.

“Viongozi wa mipango miji wajitahidi kusimamia kazi yao,waache kuwapimia wananchi maeneo ya mabondeni huko mafuriko yakitokea yanasababisha hasara kubwa ya mali kupotea na binadamu kupoteza maisha yao,

“Watu wengi wanalalamika Dar es Salaam kuchafu lakini waharibifu ni wao wenyewe hakuna mtu mwingine,tukiamua kuyatunza mazingira tunaweza kuwa na sifa kama mikoa mingine ambayo ibnasifika kwa usafi,”alisema Sadick.

Hatahivyo Sadick alisema kuwa viongozi wasimamie sheria za kutunza kwa kutimiza wajibu wao wa uwajibikaji,taasisi kuitekeleza sheria namba 20 ya mwaka 2004 kama inavyoagiza ya kutunza mazingira.

“Watendaji kupanga matumizi ya ardhi kwa uadilifu kulingana na sifa za ardhi husika mfano kutoruhusu ujenzi mabondeni,ufukweni na utengaji wa maeneo kwa shughuli mbalimbali za kijamii,

“Wananchi kutokupenda kutii sheria zilizopo kwa hiari bila shuruti,usimamizi hafifu na usioridhisha wa sheria ndogondogo na hifadhi ya mazingira,”alisema Sadick.


Pia alisema kuwa kila mwananchi wa mkoa huu watafakari kwa kina juu ya shughuli za uzalishaji wa kiuchumi zunazozingatia utunzaji wa mazingira kwani ni muhimu kuwa na mazingira endelevu kama nchi nyingine.

Aidha viongozi mbalimbali walihudhulia kwenye siku hiyo ikiwemo mkuu wa wilaya,wakurugenzi,madiwani,wenyeviti na wadau mbalimbali kutoka asasi zisizo za kiserikali.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa mtandao wa uthibiti wa mabadiliko ya tabia ya nchi (FOFUM CC), Euster Kibona, alisema wamejitahidi kufanyakazi na jamii nzima hasa katika maeneo ya mijini na vijijini kufanya shughuli za uzalishaji kwa maendeleo endelevu bila kuathiri mazingira.

Alisema kuwa maeneo ya miji ambako kuna viwanda vingi ndiko kunakoonekana kuathirika zaidi na uchafuzi wa mazingira kutokana na hewa inayotoka viwandani, maji machafu na taka nyingine nyingi.

“Kulinda na kutunza mazingira ni jukumu la mimi wewe na sisi hivyo tunatakiwa kila mmoja kuchukua hatua kuanzia sasa ili kuondokana na maginjwa yasiyotarajiwa kama vile ya mlipuko na mengine,” alisema Kibona.

No comments:

Post a Comment