Thursday, June 6, 2013

TRA kuwazungukia wafanyabiashara Dar kutoa elimu.


Na Aziza Juma, Dar es Salaam.

MAMLAKA  ya Mapato Tanzania (TRA) inatarajia kuanza mkakati wa kuwazungukia wafanyabiashara katika sehemu mbalimbali za jiji la Dar es Salaam lengo likiwa ni kutoa elimu juu ya matumizi ya mashine ya kutolea risiti.

Akizungumza na MTANZANIA jana Afisa mwandamizi wa elimu wa TRA Hamisi Lupenja ziara hiyo itaanza baada ya kumaliza semina inayoendelea  kwa wafanyabiashara hao.

Lupenja alisema mafunzo haya yanawalenga wale wafanyabiashara wenye pato la zaidi ya milioni 14 kwa mwaka na hasa wafanyabiashara ya vifaa vya ujenzi, nguo, vipuri, baa na hoteli.

“Mafunzo hayo ni kwajili ya faida kwa wafanyabiashara sio kwa TRA tu kwani inasaidia kutunza  kumbukumbu za mauzo na kudhibiti ubabaishaji wa wasaidizi wao hata wakisafiri” alisema Lupenja.

Kwaupande wake mfanyabiashara wa vipuri  Hanifa Adam aliipongeza TRA kwa hatua waliyoifanya kwani imewajengea uwelewa wa kutosha juu ya matumizi ya mashine hizo.

“Tunaishukuru TRA kwa mafunzo haya kwani yametusaidia sana katika kutumia na kujua umuhimu wa mshine hizi” alisema Hanifa.  

No comments:

Post a Comment