Thursday, June 6, 2013

TRA yawapa elimu Wawekezaji wa China.



Aziza Juma na Vick Kanje ,Dar es Saalam

AFISA mwandamizi wa  Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA )Hamisi Lupenja amewataka wawekezaji kutoka Nchi ya China   kupewa elimu ya uwekezaji wa majengo na ujenzi.

Akizungumza katika semina hiyo jana  jijini Dar es Saalm, Lupenja  alisema kuwa lengo la kutoa semina hiyo ni kutoa elimu kwa wawekezaji wa majengo na ujenzi na pia kuboresha mfumo wa kodi.

‘Tupo na jamii ya Wachina tunawapa elimu kuhusu kodi katika sekta mbalimbali ikiwemo sekta ya upangishaji na kufuata sheria za nchi.

‘Jukumu letu la msingi ni kuwapa elimu ili kuwawezesha kufanya biashara zao kwa ufanisi zaidi ’alisema Lupenja.

Lupenja alisema kuwa wameshafanya semina nyingi na sehemu mbalimbali ikiwemo semina kutumia machine ya Electronic kwa wafanyabiashara .

Alisema kuwa wapotayari kukumbana na changamoto wakati wa utoaji elimu kwa wafanyabiashara na kuna baadhi ya wafanyabiashara wanaojua kutumia mashine hizo lakini wanakuwa wabishi kutumia wakidai hawajui jinsi ya kutumia .

MWISHO.

Hata hivyo alisema kuwa wanatoa elimu kwa wafanyabiashara wote bila kujali ni Mchina au Mtanzania. 

No comments:

Post a Comment